Katika tukio hilo, mmoja anayesadikiwa kuhusiana na watu hao 
waliokamatwa aliuawa na wananchi wenye hasira baada ya kumjeruhi kwa 
panga askari polisi aliyekuwa akipambana naye.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa polisi mkoani 
Morogoro, Leonald Paul alisema tukio hilo lilitokea juzi (Aprili 14 
mwaka huu) majira ya saa 3.30 usiku katika kitongoji cha Nyandero, 
tarafa ya Kidatu wilayani Kilombero.
Kamanda Paul alimtaja mtu aliyefariki kuwa ni Hamad Makwendo ambaye umri
 wake haujafahamika ambaye ni mkazi Manyasini Ruaha wilayani Kilombero.
Aidha alisema siku ya tukio polisi walipata taarifa kutoka kwa raia wema
 kuhusu watu hao na kwamba walitaarifiwa kuwa wanajihusisha na matukio 
mbalimbali ya uhalifu na polisi waliamua kufatilia nyendo zao.
Akisimulia tukio hilo, Kamanda Paul alisema: “Polisi walipata taarifa 
kuwa watu hao walitumia usafiri wa bajaji mbili kwenda kusikojulikana na
 wakati wakiendelea na zoezi la kufuatilia ndipo walikutana na bajaji 
moja ikiwa na abiria mmoja ambaye ni Mkwendo na kuisimamisha.”
Alisema kuwa bajaji hiyo iliposimama marehemu huyo aliruka na kuanza 
kukimbia ndipo askari mwenye namba F .3323 Koplo Nasoro alianza 
kumkimbiza na alipomkaribia mtuhumiwa huyo alichomoa jambia alilokuwa 
nalo na kumkata askari huyo eneo la shingoni.
Askari mwingine mwenye namba E.9245 Koplo Chomola ambaye alikuwa nyuma 
alifanikiwa kumpiga risasi ya mguu mtuhumiwa huyo,ambapo alipoanguka 
chini wananchi wa eneo hilo tayari walifika katika eneo hilo na kuanza 
kumshambulia marehemu huyo kisha kumchoma moto kwa hasira.
Kamanda huyo alisema walianza kuwasaka watu wengine ambao walipata taarifa wapo katika Msikiti wa Suni uliopo Kidatu.
“Polisi walipofika katika msikiti huo waliuomba uongozi wa msikiti huo 
kuwatoa watu wote waliokuwa msikitini ili kuweza kubaini watu ambao 
wanatiliwa mashaka,”Alisema kamanda  Paul
Alisema polisi waliendelea na ukaguzi na kuwakamata watu hao 10 wakiwa na vifaa hivyo na kuwatia nguvuni.
 











 
 
0 comments:
Post a Comment